Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Balozi wa Afrika Kusini asifia hatua ya Zanzibar

12/11/2009

AFRIKA Kusini imeeleza kuridhishwa na mazungumzo kati ya rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Amani Abeid Karume na Seif Sharrif Hamad ambaye ni katibu mkuu wa CUF na kueleza kuwa hatua hiyo ni changamoto kwa bara la Afrika.

Afrika Kusini pia imeeleza kuwa hatua ya viongozi hao wawili wa vyama vyenye upinzani mkubwa kwenye visiwa hivyo, imeonyesha kukua kwa demokrasia.

Balozi wa Afrika Kusini, Sindiso Mfenyana, ambaye anamaliza muda wake nchini, alisema hayo jana wakati alipokuwa na mazungumzo na Rais Karume Ikulu mjini Zanzibar.

Balozi Mfenyana alimueleza Rais Karume kuwa hatua hiyo ni somo kubwa kwa nchi za barani Afrika, ikiwemo nchi yake ya Afrika Kusini kwani kilichozingatiwa zaidi ni maslahi ya wananchi na nchi yao.

Mfenyana alieleza kuwa Afrika Kusini itaendelea kuimarisha uhusiano na udugu wake na Zanzibar na kusisitiza kuwa hatua hiyo ina matarajio makubwa ya kusonga mbele kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Alieleza kuwa mazungumo hayo yanatoa faraja kubwa na ni imani yake kwamba Zanzibar itaendelea kupiga hatua kubwa katika maendeleo yake, ikiwa ni pamoja na miradi ya maendeleo sanjari na kuimarisha amani na utulivu uliopo.

Alisema kuwa hatua ya kukaa kwa pamoja kati ya viongozi hao imeudhihirishia ulimwengu kuwa Wazanzibari wote ni wamoja na tofauti zao za kisiasa haziwezi zikawatenganisha.

Habari na Salma Said, Zanzibar.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©