Mjadala wa soko la pamoja
Afrika Mashariki
22/11/2009

Viongozi
wa kuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Toka shoto ni Marais Yoweri
Museveni wa Uganda, Mwai Kibaki wa Kenya, Paul Kagame wa Rwanda, Jakaya
Kikwete wa Tanzania na Pierre Nkurunzinza wa Burundi.
Ijumaa
ilopita Jumuiya ya Afrika Mashariki ilitimiza miaka 10 ya uhai wake na
viongozi wakuu watano wote walikuwa jijini Arusha katika hitimisho la
sherehe hizo zilizoambatana na utiwaji saini makubaliano ya kuwa na soko
la pamoja na pia kuwekwa kwa jiwe la msingi la makao makuu ya jumuiya
hiyo yanayojengwa jijini humo.
Si
vibaya kujadili umuhimu wa tukio hilo la kihistoria la kuwa na soko la
pamoja kwa nchi hizo tano utaoanza kutumika rasmi Januari 1, 2010, hatua
ambayo itafuatia kuwa na sarafu ya pamoja na, endapo pande zote
zitakubaliana, hatimaye shirikisho la Afrika Mashariki.
|