Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Magari ya wizi yakamatwa Tanzania

02/12/2009

JESHI la polisi nchini kwa kushirikiana na ofisi za Interpol Kanda ya Kusini mwa Afrika (SARPCCO) wameendesha operesheni maalum ya siku mbili inayojulikana kama “NAMUTUNI” nchi nzima na kukamata watuhumiwa 110, na vielelezo mbalimbali yakiwemo magari 54 yaliyoibwa nchi tofauti.

Polisi pia wamekamata pikipiki sita, nne kati ya hizo ziliibwa nchini Kenya.

Magari 48 kati ya waliyokamatwa yaliibwa nchi mbalimbali ikiwemo matatu Afrika Kusini, 38 Japan, magari manne England, na moja moja katika nchi za Jamuhuri ya Dominic, Australia na Kenya.

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba, ameyasema hayo katika taarifa iliyosomwa na Kamishna wa polisi, Dominic Hayuma wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam.

Amesema, operesheni hiyo ilifanyika Novemba 23 hadi 25 na ilifanikisha kukamata dawa za kulevya zikiwemo kete 28 za Heroine, kilo 608 za mirungi, ekari 6 na kilogramu 801,335 za bangi, na misokoto 40 ya bangi.

“Pia tulikamata silaha mbalimbali zikiwemo bastola mbili, gobore moja, mabomu mawili ya kutupa kwa mkono, magazine 11, SMG nne na risasi zake 607 pamoja na wahamiaji haramu (wa kinyume na sheria) 25 kutoka nchi za Ethiopia, Burundi, Marekani, Jamaica na DRC” amesema Manumba katika taarifa hiyo.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©