Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Waziri Batilda atembelea kiwanda cha Bakhresa

05/12/2009

Pichani kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Dk. Batilda Burian akionyeshwa chembe chembe za chupa zilizosagwa katika mtambo maalum na Meneja Mitambo Bw Jones Solomon alipotembelea kiwanda cha kusaga taka za chupa cha Kampuni ya Bakhresa kilichopo Chang'ombe jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Dk. Batilda S. Burian ametembelea Kiwanda cha kurejeleza (recycle) chupa za plastiki cha Bakharesa kilichopo Chang’ombe jijini Dar es Salaam.

Mh. Dk. Batilda amesema amefarijika kuona kuwa sasa kuna Kiwanda cha kurejeleza chupa ambazo zilikuwa uchafu na kero katika Miji hususan jijini Dar es Salaam.

Mhe. Dkt. Batilda amepongeza Kampuni ya Bakhresa kwa ukusanyaji chupa na kuzirejeza. Amesema kuwa urejelezaji wa chupa hizi utasaidia katika kupambana na uchafuzi wa mazingira na kusaidia kuwapa kipato wauzaji wa chupa za plastiki zilizotumika.

Alisema chupa nyingi zinazoletwa ni chafu kwa hiyo zinahitaji kusafishwa katika mtambo maalum uliopo kiwandani ambapo bidhaa inayozalishwa huwa salama. Mhe. Dk. Batilda amesema Serikali tutaendelea kuhimiza utengaji wa taka hivyo kuweza kurahisisha urejelezaji.

Mhe. Dk. Batilda alisema kuwa Ofisi yake itahahakikisha kuwa vinaanzishwa vituo vya kukusanya chuo hizo na kuleta Kiwandani na watalipwa pesa zao.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©