Wawili wapata tiketi ya
mkutano wa 'Climate Change'
06/12/2009

Pichani kushoto ni Balozi wa UK nchini
Tanzania, Diane Corner, akimkabidhi bwana Lucas Liganga mfano wa tiketi
ya kwenda Copenhagen kwenye mkutano wa 'Climate Change'. Tiketi hiyo
imetolewa baada ya wishindi hao kushida katika mashindano maalum ya
uandishi ambayo washiriki mbalimbali walijihusisha kuandika athari za
'Climate Change'.

Pichani kulia ni Balozi wa UK nchini
Tanzania, Diane Corner, akimkabidhi bwana Timothy Kitundu mfano wa
tiketi ya kwenda Copenhagen kwenye mkutano wa 'Climate Change'. Tiketi
hiyo imetolewa baada ya wishindi hao kushida katika mashindano maalum ya
uandishi ambayo washiriki mbalimbali walijihusisha kuandika athari za
'Climate Change'.
Washindi hao wameshinda tiketi hizo za
kuhudhuria mkutano wa Climate Change Conference (COP15) mjini Copenhagen
mwaka huu. Bwana Liganga aliingia katika mashindano hayo na maandishi
aliyoyaita "Climate Change: Over One million Tanzanians are at Risk of
Starvation, Crops are Failing".
Na bwana Kitundu aliingia katika
mashindano hayo na maandishi aliyoyaita "Climate Change Impact in
Tanzania: Severe Strees in Social Structure". Mwingine ambaye alikuwa ni
mshindi wa mwisho lakini hakupata nafasi ya tiketi bi Sharifa Kalokola
aliingia na maandishi aliyoyaita "As Temperatures Rise, Malaria Deaths
Soar".
Balozi Diane amesema, ameona ni muhimu
matatizo ya Tanzania yahudhuriwe na yaelezwe na Watanzania wenyewe na
Ubalozi huo umefurahi kudhamini mashindano hayo.
|