Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

JUMUIA YA AFRIKA MASHARIKI KUFUNGWA MPAKA MWAKANI

14/12/2009

Jumuia ya Afrika ya Mashariki (EAC) katika mwaka ujao itakabiliwa na changamoto kubwa za kuhakikisha inaondoa kero wakati wa kuanza kwa Umoja kamili wa Forodha na pia kuhakikisha nchi wanachama zina ridhia kwa wakati muafaka itifaki ya kuanzishwa kwa soko la pamoja.

Hayo yamebainishwa na katibu mkuu wa jumuia ya Afrika ya mashariki Balozi Juma Mwapachu wakati wa salamu zake za kuuaga mwaka huu wa 2009 kupitia vyombo vya habari ambapo jumuia hiyo imefunga shughuli zake mpaka mwezi Januari Mwakani.

Balozi Mwapachu alisema kwa Marais Jakaya Kikwete (Tanzania) Yoweri Museven (Uganda), Mwai Kibaki (Kenya), Paul Kagame (Rwanda) na Pierre Nkurunziza (Burundi) kusaini itifaki wa Soko la pamoja mwezi uliopita sasa itakuwa kazi ya mabunge ya nchi hizo kuridhia itifaki hiyo.

Alisema kuwa utekelezaji wa soko la pamoja unatakiwa kuanza kwa kasi katika kuelekea kwenye hatua inayofuata ya kuwa na sarafu moja ya Afrika ya mashariki.

Aidha Balozi Mwapachu alisema katika mwaka huo nchi hizo zitakuwa na jukumu la kuandaa mpango mkakati wa nne wa jumuia ya Afrika ya Mashariki wa mwaka 2011 na 2016 utakaolenga katika kuandaa programu za kiuchumi,ushirikiano wa kisiasa pamoja na sekta za kijamii.

Balozi Mwapachu alisema umekuwa na mafanikio makubwa hasa katika katika kupitishwa kwa sera muhimu na uboreshaji wa miundombinu. Alisema kuwa katika sera kubwa za pamoja zilizopitishwa zilikuwa ni pamoja na mikakati ya uboreshaji wa barabara,reli,usafiri wa maji na anga,bandari,mawasiliano ya simu,nishati na usalama wa anga.

Balozi Mwapachu alisema kuwa mafanikio makubwa yalipatikana katika barabara baada ya kuzinduliwa kwa ujenzi wa barabara kati ya Arusha-Nambanga hadi Athi River Mapema mwezi Machi na wakuu wa nchi hizo katika eneo la Lengijave wilayani Arumeru mkoani hapa.

Alisema barabara hiyo ni muhimu katika kuunganisha kati ya Kenya na Tanzania mpaka Unganda na baadhi ya maeneo ya Rwanda na Burundi. Balozi Mwapachu alitaja mradi mwingine ni wa kuunganishwa nguvu ya umeme kati ya Kenya na Tanzania katika mpaka wa Namanga.

Mipango mingine ni pamoja na Mradi wa Kilimo na program za maendeleo vijijini,program za maendeleo za Bonde la ziwa Victoria. Alisema pia katika mwaka huu kumekuwepo na kazi kubwa ya ya kuhamasisha eneo hilo kuwa la soko la pamoja na uwekezaji ambapo mkakati huo ulikamilika kwa nchi hizo kukamilisha mchakato na hivyo kuanza rasmi kwa umoja wa forodha ifikapo Januari mosi mwakani.

Balozi Mwapachu alitumia fursa hiyo kuwashukuru wakuu wa nchi zote tano zinazounda jumuia hiyi,baraza la mawaziri pamoja na asasi zote na taasisi za jumuia hiyo pamoja na wafanyakazi wote kwa kufanikisha malengo ya kazi za jumuia.

Aidha Balozi Mwapachu amewashukuru wadau wengine wa karibu ndani ya jumuia hiyo likiwemo baraza la Biashara la Afrika ya Mashariki,wananchi panoja na washirika wa maendeleo wa jumuia hiyo kwa kutoa misaada mbalimbali ya hali na mali.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©