Abdulhakim (Kim) afariki
dunia
17/12/2009

Abdulhakim Magomelo (pichani kushoto)
maarufu kwa jina la (Kim) amefariki dunia tarehe 16/12/2009 kwenye
hospitali ya binafsi inayoshughulika na magonjwa ya moyo iliyopo Manzese,
Dar es Salaam. Taarifa hiyo ilitolewa na shemeji yake bwana Muddy
Bawazir.
Abdulhakim ni mmoja wa vijana aliyechangia
katika fani tofauti nchini Tanzania na zaidi atakumbukwa na vijana
aiyewapa fursa na kuichukua fursa hiyo kwa kuitumia kwa njia nzuri
katika maisha yao.

Abdulhakim amezikwa makaburi ya Kisutu
jijini Dar es Salaam hii leo saa kumi na moja Alasir baada ya mwili wake
kuchukuliwa kutoka nyumbani kwake mtaa wa Mkwepu kuelekea msikiti wa
Ngazija, mtaa wa Makunganya, Dar es Salaam, kwa kuswaliwa swala ya maiti
na kuelekea makaburi ya Kisutu. Mola amsemehe madhambi yake na
amghufirie adhabu za kaburini na kesho akhera. Amen.
|