Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Yanga yailaza Simba mabao 2-1

24/12/2009

Timu ya Yanga a.k.a Watoto wa Jangwani imemkung'uta mtani wake wa jadi Simba kwa mabao 2-1 kwenye nusu fainali za kombe la Tusker Cup. Watani wemetangaza magoli hayo kama ni zawadi nono ya Krismas kwa wapenzi wake. Alikuwa ni Jerry Tegete aliyeweka chuma kimiani zikiwa zimebaki dakika tatu kabla ya muda wa dakika 120 kumalizika.

Mpaka dakika 90 kwisha, mpira ulikuwa nguvu sawa baina ya timu zote mbili kwa kutoka droo (1-1), ndipo zilipoongezwa dakika 30 za mwisho za kutafutwa mshindi wa kombe hilo. Kocha wa Yanga pichani akisisitiza jambo kwa kuwashajiisha vijana wa mjini waweke kandambili pembeni, wavae njuga za kumlisha vidonge mtani wao wa jadi Simba.

Kocha wa Yanga Kostadic Papic, au kwa jina lingine akijulikana kama 'Clinton'.

Kocha wa Simba Patrick Phiri.

Washabiki wa Yanga wakishangilia katika jukwaa wakati wa mchezo huo na watani wa jadi.

Washabiki wa Simba wakishangilia katika jukwaa wakati wa mchezo huo na watani wa jadi.

Kocha wa Yanga Kostadic Papic 'Clinton' akiwa kabebwa na mashabiki kwa kuiwezesha timu yao kuwashinda watani wa jadi Simba kwa mabao 2-1.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©