China yazindua treni ya
kwanza kwa kasi duniani
27/12/2009

Baada ya Olimpiki ya mwaka 2008, China
imekuwa katika kasi ya kuimarisha miundombinu ya usafiri na njia
mbalimbali za maendeleo kulingana na kasi ya uchumi wa nchi yake.
China imezindua rasmi treni yake (bullet
train) ambayo inajulikana kwa jila la 'Harmony Express' inasemekana
inakwenda mbio kuliko treni yoyote duniani, imepita ile ya Japan na ya
France; treni hiyo ya kipekee ambayo inaunganisha miji miwili ya kisasa
iliyopo China ya Guangzhou na Wuhan kwa mbio za Kilomita 350 kwa saa
(217miles per hour).
Treni hiyo itasaidia kupunguza muda wa
usafiri wa kutoka mji mmoja mpaka mwingine kwa masaa matatu na nusu.
Safari ya miji hiyo miwili kabla ya treni hii kuanza kazi huchukua muda
wa masaa 7.5 (saba na nusu), lakini sasa inachuku masaa (3) matatu.
Kazi ya treni hiyo imeanza tangu mwaka
2005 kurahisisha safari za miji miwili hiyo ikiwamo Guangzhou, ambao ni
mji mmoja wapo wa kisasa na ni mji mmoja wapo kama ni kitovu cha
biashara uliopo kusini mwa China karibu na Hong Kong.
Wanamamlaka wa China wamesema, treni hiyo
ina uwezo wa kwenda mpaka Kilomita 394.2 kwa saa; na wameshapania
kujenga barabara 42 za treni hiyo kuunganisha vitongoji na miji tofauti
nchini China ifikapo mwaka 2012.
|