Mafuriko yaikumba Kilosa
30/12/2009

Baadhi
ya vijana wa eneo la Kata ya Kasiki na Mbumi wa Mjini Kilosa, wakibeba
kichwani mwao godoro kuepusha lisiloane na maji ya mafuriko kutoka mto
Mkondoa yaliyotokea asubuhi ya Desemba 26, mwaka huu mjini humo kufuatia
mvua zilizonyesha katika milima iliyopo Wilayani Mpwapwa na Kongwa, Mkoa
wa Dodoma kuanzia wiki ya Krismas.

Ng’ombe
walioletwa machinjioni kwa ajili ya kuchinjwa wakiwa wamezingirwa na
maji ya mafuriko yaliyotokea asubuhi ya Desemba 26, mwaka huu mjini
Kilosa.

Jengo la
machinjio la Mji wa Kilosa likiwa limezingirwa na maji ya mafuriko na
hivyo kusababisha ng’ombe walioletwa kwa ajili ya kuchinjwa siku hiyo ya
Desemba 26, mwaka huu kushindwa kuchinjwa kutokana na eneo hilo kujaa
maji.

Baadhi
ya vifaa vya wakazi wa Kata ya Kasiki na Mbumi za Mjini Kilosa vikiwa
vimetolewa nje ya nyumba zao ili visisombwe na maji ya mafuriko
yaliyotokea Desemba 26, mwaka huu mjini humo.

Gari
aina ya Fuso lenye namba T 952 ABZ likiwa na magunia ya nafaka
zilizookolewa kwenye moja ya nyumba iliyokumbwa na mafuriko Desemba 26,
mwaka huu likijaribu kulivuta Gari jingine lililokwama eneo la mitaa ya
Kata ya Kasiki, baada ya kutitia kutokana na kujaa kwa maji Barabarani
kufuatia mto Mkondoa kufurika.

Diwani
wa Kata ya Kasiki katika Mji wa Kilosa, Ahamed Islam (kushoto) na
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, Ephrem
Kalimalwendo, (kulia) kwa pamoja wakimwongoza Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,
Issa Machibya (nyuma kulia) kuweza kuangalia baadhi ya maeneo ya mji wa
Kilosa yaliyokumbwa na mafuriko ya maji asubuhi ya Desemba 26, mwaka huu.

Mkazi wa
Kata ya Mbumi akiwa kabeba mikononi Cherehani yake kuepusha isiharibiwe
na maji ya mafuriko yaliyotokea asubuhi ya Desemba 26, mwaka huu mjini
humo baada ya mvua kubwa zilizonyesha kwenye milima iliyopo Wilayani
Mpwapwa na Kongwa, Mkoa wa Dodoma kuanzia wiki ya sikukuu ya Krismas na
kusababisha mto Mkondoa kufurika.

Wakazi
wa nyumba moja iliyokumbwa na mafuriko wakiwa nje ya ya nyumba yao
wakitafakari jinsi ya kujiokoa pamoja na mali zao zilizokuwemo ndani
kama walivyokutwa eneo hilo asubuhi ya Desemba 26, mwaka huu mjini
Kilosa.
|