Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Mzee Rashid Mfaume Kawawa afariki dunia

01/01/2010

Mzee Rashid Mfaume Kawawa amefariki dunia jana siku ya Alhamisi ya tarehe 31/12/2009 katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikolazwa tokea jana baada ya kupata matatizo ya kiafya. Mzee Rashid Mfaume Kawawa alijulikana kwa jina lingine kama "simba wa vita" alizaliwa Liwale, Dar es Salaam, mwaka 1926 ambapo baada ya kushika nyadhifa mbalimbali alikuwa Waziri Mkuu kuanzia Januari 22, 1962 hadi Februari 13, 1977 akifuatiwa na hayati Edward Moringe Sokoine, baadaye aikuwa Katibu Mkuu wa CCM kabla ya kustaafu kwake.

Picha zifuatazo ni picha zake mbalimbali ambazo zilichukuliwa katika uhai wake. Juu pichani akiwa na na Rais Jakaya Kikwete akiongea jambo na Mzee Rashid Kawawa katika mojawapo ya picha za mwisho za kutumikia taifa wakati wa uhai wake.

Mzee Kawawa akiwa na mkewe bungeni Dodoma, pamoja na utu uzima wake daima alikuwa mstari wa mbele kulitumikia taifa katika uhai wake.

Mzee Kawawa akitunukiwa tuzo ya Amani ya Martin Luther King na aliyekuwa balozi wa Marekani nchini Tanzania.

Mzee Kawawa alikuwa hakosekani kwenye vikao muhimu vya chama chake pale alipoalikwa katika kutumikia taifa wakati wa uhai wake.

Mzee Kawawa akiwa mgeni rasmi kwenye onesho la Miss Tanzania ambapo mshindi alikuwa Richa Adhia, katikati pichani.

Mzee Kawawa aliyesimama pili kutoka kushoto, akiwa katika baraza la kwanza la Mawaziri Tanganyika mara baada ya uhuru mwaka 1961. Katika baraza hilo, Mzee Kawawa ndiye aliyekuwa peke yake amebaki hai kati ya waasisi hao mpak kufa kwake jana tarehe 31/12/2009; Mungu atulindie taifa letu. Amen.

Mzee Kawawa (watatu kulia) na Mwalimu Nyerere (wanne kulia) wakiwa pamoja na Wakuu waliopigania uhuru akiwa katika tafrija ya kusheherekea uhuru wa Tanganyika mwaka 1961.

Mzee Kawawa akiwa na Mwalimu Nyerere na aliyekuwa Rais wa Zanzibar enzi hizo Mzee Aboud Jumbe huku Rais wa Msumbiji, Samora Machel akiangalia.

Mzee Kawawa akiwa na Mwalimu pamoja na kiongozi wa dini wa dhehebu la Ismailia duniani, H.H. Aga Khan.

Akiwa kama kiongozi wa vitendo, Mzee Kawawa alikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kujiunga na jeshi la kujenga taifa kwa mujibu wa sheria mara tu lilipoanza rasmi.

Mzee Kawawa akiwa na timu ya taifa, Taifa Stars.

Mzee kawawa alikuwa mpenzi mkubwa wa michezo ya mpira wa miguu na hapa akiwa kama refa katika mchezo wa Wabunge na Mawaziri wakati wa uhai wake.

Tarehe 31/12/2009 Mzee Kawawa afariki dunia; rasmi Rais wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete alitangaza kifo hicho kwa waandishi wa habari waliokusanyika ikulu, Dar es Salaam. Rais ametangaza pia siku saba za maombolezo kitaifa ambapo bendera zitapepea nusu mlingoti nchi nzima.

Rais Jakaya Kikwete akiongea na mwanasiasa mkongwe, Mzee Kingunge Ngombare Mwiru baada ya kutangaza rasmi kifo cha Mzee Rashid Mfaume Kawawa Ikulu Dar es Salaam.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, William Lukuvi akimpa pole Mh. Vita Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, Songea, ambaye mtoto wa Marehemu Rashid Kawawa nyumbani kwa marehemu, Madale, jijini Dar es Salaam jana jioni.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, William Lukuvi akimfariji mke wa Marehemu Rashidi Mfaume Kawawa, Asina Kawawa, wakati alipoitembelea familia ya marehemu nyumbani kwa marehemu, Madale, jana jioni.

Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba (kushoto) akimlilia Mzee Rashid Kawawa wakati alipokwenda nyumbani kwa marehemu, Madale, jijini Dar es Salaam jana jioni.

Mzee Yusuf Makamba akimfariji Zainab Kawawa mtoto wa marehemu Rashidi Kawawa, Madale, jana jioni.

Leo tarehe 01/01/2010, Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete walikwenda kutoa heshima za mwisho kwa marehemeu Mzee Rashid Mfaume Kawawa katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam jioni hii. Mamia ya wananchi wamefurika ukumbini hapo kumuaga Mzee Kawawa anayetarajiwa kuzikwa nyumbani kwake Madale kesho Jumamosi.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete wakiifariji familia ya Marehemu Mzee Rashid Mfaume Kawawa muda mfupi baada ya kutoa heshima za mwisho.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©