Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Mzee Rashid Mfaume Kawawa azikwa leo

02/01/2010

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha Maombolezo wakati alipowasili nyumbani kwa Marehemu Mzee Rashid Mfaume Kawawa kushiriki katika mazishi yake yaliyofanyika nyumbani Kwake madale jijijni Dar es Salaam.

Mzee Rashid Mfaume Kawawa amefariki dunia siku ya Alhamisi ya tarehe 31/12/2009 katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikolazwa baada ya kupata matatizo ya kiafya. Mzee Rashid Mfaume Kawawa alijulikana kwa jina lingine kama "simba wa vita" alizaliwa Liwale, Dar es Salaam, mwaka 1926 ambapo baada ya kushika nyadhifa mbalimbali alikuwa Waziri Mkuu kuanzia Januari 22, 1962 hadi Februari 13, 1977 akifuatiwa na hayati Edward Moringe Sokoine, baadaye aikuwa Katibu Mkuu wa CCM kabla ya kustaafu kwake.

Maafisa wa jeshi wakiwasili kaburini tayari kwa maziko ya Mzee Rashid Mfaume Kawawa.

Maafisa wa Jeshi wakijiandaa kubeba jeneza.

JK akiongoza sala ya maiti akiwa na viongozi wengine wakuu.

Mh. Vita Kawawa (mtoto wa Rashid Mfaume Kawawa) akiwa amejitwisha jeneza lenye mwili wa marehemu baba yake kuelekea kaburini.

Mkuu wa majeshi mstaafu Jenerali George Waitara (shoto) akiwa na maafisa wa ngazi za juu msibani.

Mzee Songambele akiwa na Mheshimiwa Vita Kawawa.

Mawaziri Wakuu wastaafu msibani.

Baadhi ya waombolezaji waliofika mazikoni.

Baadhi ya waombolezaji waliofika mazikoni.

Hema kuu likiwa na viongozi mbali mbali waliohudhuria katika maziko hayo.

Baadhi ya waombolezaji waliofika mazikoni kumpa heshima ya mwisho Mzee Kawawa.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka mchanga kaburini wakati wa mazishi ya Mzee Rashid Mfaume Kawawa huko Madale jijini Dar es Salaam leo.

Makamu wa Rais Dk. Ali Mohamed Shein akiweka mchanga kaburini.

Wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama wakijipanga tayari kuweka mchanga kaburini.

Heshima za mwisho za kijeshi zilihitimishwa na mizinga 19 (kumi na tisa) wakati huo.

Heshima za mwisho za kijeshi.

Kikosi cha Buruji, kikiliza "the last post".

Shekhe Mkuu Issa Shaaban Simba akiongea msibani. Alisisitiza umuhimu wa historia za watu kama Mzee Rashid Mfaume Kawawa "Simba wa Vita" kuandikwa na kuhifadhiwa ili kuwaenzi milele.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©