Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Burj Khalifa lafunguliwa rasmi

04/01/2010

JENGO refu duniani kwa sasa rasmi ni Burj Khalifa baada ya kuzinduliwa leo kwa mbwembwe za fataki na mataa ya kung'ara, linajidai kwa kusimama urefu wa zaidi ya mita 800 (mia nane) kushinda jengo la Taipei 101 ambalo lilisemekana kuwa ni jengo refu duniani kabla ya Burj Khalifa kuzinduliwa. Mengine maarufu yanayofuatia ni Petronas Towers, Sears Tower, Empire State na Canary Wharf la London.

Anga za Dubai zikimulikwa na cheche zinazotoka kwenye jengo la Burj Khalifa mara baada ya uzinduzi rasmi wa jengo hilo kufunguliwa kuashiria kuwa jengo hilo ndio refu kuliko yote duniani na vilevile kuashiria Dubai inaongoza kwa majengo ya kisasa. Sheikh Mohammed Al Maktoum (Mtawala wa Dubai) alifungua rasmi jengo hilo baada ya kuvuta kipazia cha ukutani na kuwatangazia umati uliokusanyika jina la jengo hilo kuwa ni 'Burj Khalifa'. Katika ufunguzi huo, baadhi ya waliohudhuria hapo walichukuliwa na mshangao wa muda baada ya kusikia jina la jengo hilo ni 'Burj Khalifa' badala ya 'Burj Dubai'.

Baadhi ya wakazi wa Dubai wakipita mbele ya jengo la 'Burj Khalifa' kabla ya usiku wa jengo hilo kufunguliwa rasmi.

Ni rasmi, jengo refu kuliko lote duniani kwa sasa ni Burj Khalifa ambalo lilikuwa likijulikana kama Burj Dubai kabla ya uzinduzi wake.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©