Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Maombolezo ya Mzee Rashid Mfaume Kawawa - London

05/01/2010

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania waishio UK, Ndugu Abubakar Faraji akiweka sahihi yake. Kwa majonzi makubwa amesema jina la Simba wa Vita halikuja hivi hivi na kwamba ni kweli Mzee Rashidi Mfaume Kawawa alikuwa Simba wa Vita vyote vya Tanganyika na baadaye Tanzania, akisimama kidedea katika shida na raha zote nchi ilipitia. Na kwamba endapo Mwalimu Nyerere alikuwa wino basi Mzee Kawawa alikuwa kalamu na kwa pamoja waliweza kuiandika historia ya kipekee ya Tanzania ambayo ni kisiwa cha upendo, amani na utulivu kutokana sio tu na busara zao bali pia kwa kuona mbali na kuunganisha matabaka yote.

Balozi wa Ghana, Profesa Kwaku Danso-Boafo akiweka sahihi na kusema "Afrika imempoteza kiongozi wa kipekee. Bwana Kawawa alikuwa kiongozi aliyetutia hamasa wanasiasa wengi Afrika, wengi wetu tuliingia kwenye siasa kwa kufuata nyayo zake. Alichangia kiasi kikubwa kwa ukombozi wa Afrika."

Balozi wa Papua New Guinea, Bi Jean L Kekedo, O.B.E. akiweka sahihi yake. Amesema "Tunatoa pole kwa kifo cha kiongozi huyu mkuu."

Balozi wa Zambia, Profesa Royson Mukwewa akiweka sahihi yake. Yeye alimwelezea Mzee Kawawa kama "Shujaa Mkuu wa Tanzania na Afrika aliyejitolea muhanga kupigania ukombozi wa Bara zima." Alisema njia pekee ya kumuenzi Mzee Kawawa ni kuendeleza yale aliyoyapigania wakati wa uhai wake.

Balozi wa Zimbabwe, Mhe. Gabriel Machinga (Picha ya juu) amesema "Tunashukuru kwamba Mzee Kawawa ameacha historia iliyovuka mipaka ya nchi yake na bara zima la Afrika. Atakumbukwa sana na wengi tunamshukuru kwa kazi aliyoifanya."

Mtoto wa mdogo wa Simba wa Vita ambaye pia ni wajina wake, Rashidi Kawawa, akiweka sahihi kwenye kitabu cha maombolezo. Hitma imeandaliwa siku ya Jumamosi kuomboleza kifo cha Mzee Rashid Mfaume Kawawa.

Bendera ya Tanzania ikipepea nusu mlingoti ubalozini London, UK.

Hitma ya Mzee Rashid Mfaume Kawawa itafanyika Jumamosi ya tarehe 09/01/2010, St Anns Mosque, St Anns Road, Tottenham, London, N15 5GJ, SAA 9 JIONI.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©