Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Mafuriko ya Kilosa

09/01/2010

Waziri Mkuu Mizengo Pinda (kulia) akimtambulisha Waziri wa Tamisemi, Celina Kombani (kushoto) mbele ya waathirika wa mafuriko yaliyozikumba Kata nane za Wilaya ya Kilosa wanaoishi katika kambi ya muda ya shule ya Msingi Kondoa, wakati Waziri Mkuu walipowatembelea kuwapa pole waathirika hao.

Waziri wa Miundombinu, Dk Shukuru Kawambwa (watatu kutoka kushoto) akizungumza jambo na Waziri wa Tamisemi, Celina Kombani (wapili kutoka kushoto) kuhusiana na athari za kibinadamu na miundombinu kabla ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuwahutubia waathirika wa mafuriko waliopo kwenye kambi ya muda ya shule ya Msingi Kondoa; wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu, Omary Chambo.

Pichani ni sehemu ya kambi ya muda ya waathirika wa mafuriko Kilosa.

Pichani ni sehemu ya kambi ya muda ya waathirika wa mafuriko Kilosa.

Wananchi wakivuka mto Mkondoa katika mafuriko yaliyokumba mto huo Kilosa.

Daraja la reli ya kati iliyokumbwa na madhara ya mafuriko hayo.

Barabara ya Reli ikionekana pichani ikining'inia baada ya daraja la reli hiyo kuvunjika baada ya kukumbwa na madhara ya mafuriko.

Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkullo (kushoto) akipitia orodha ya vifaa vya misaada ya dawa za binadamu na mingine iliyotolewa na Mkurugenzi wa Hospitali ya Regency ya Dar es Salaam iliyowasilishwa kwa Mbunge wa Jimbo la Kilosa ikiwa ni kuwasaidia waathirika wa mafuriko yaliyotokea mjini Kilosa kuanzia mwishoni mwa mwaka jana.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©