Karume azindua barabara
mpya Pemba
11/01/2010

Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Amani Abeid Karume, akisalimiana
na Katibu Mkuu wa CUF, Seif Sharif Hamad, alipowasili katika uwanja wa
Mkutano wa Makombeni jana. Mkutano ulizungumzia zaidi umoja na utulivu
Nchini, katika kusherehekea miaka 46 ya Mapinduzi Zanzibar.

Wananchi wa Makombeni Mkoa
wa Kusini Pemba, wakimsikiliza Rais Karume alipozungumza nao wakati wa
Mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa mpira Makombeni,
miongoni mwa shamra shamra za miaka 46 ya Mapinduzi Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Amani Abeid Karume, akikata utepe
ikiwa kama ishara ya uzinduzi wa Barabara ya MKoani, Makombeni Pemba,
katika kusheherekea miaka 46 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Amani Abeid Karume na Waziri wa
Mawasiliano na Uchukuzi Machano Othman Saidi, pamoja na Viongozi wengine,
wakitembea katika Barabara ya mkoani, Makombeni, iliyojengwa na nguvu za
Serikali, mara baada ya kuizindua ikiwa ni sherehe za kuadhimisha miaka
46 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
|