Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Mtetemeko wateketeza Haiti

13/01/2010

Mtetemeko wa ardhi wenye ukubwa wa nguvu 7.0 umeuteketeza Haiti nchi ambayo ipo katika visiwa vya Caribbean, Kusini mwa Marekani ya Kaskazini. Mtetemeko huo umesababisha maelfu ya majumba kuvunjika yakiwemo mahospitali na makazi ya watu ambao wameachwa bila ya makazi na kadiri ya watu laki moja wasadikiwa wamekufa baada ya mtetemeko huo kutetemesha ardhi ya Haiti jioni mwa Jumanne ya tarehe 12/01/2010.

Mtetemeko huu haujawahi kutokea katika nchi hiyo zaidi ya miaka 200 iliyopita ilisabibisha nchi kuingia katika usiku wa giza baada ya nchi kukosa umeme, simu, maji, chakula na hata matibabu ya waliokumbwa na mtetemeko huo.

Haiti ni moja ya nchi masikini duniani na ni nchi pekee maskini katika nchi ambazo zipo Kaskazini mwa dunia. Pia ni nchi ambayo kihistoria inajulikana kwa kutokuwa na utulivu wa kisiasa. Mara baada ya mtetemeko huo kutingisha nchi hiyo, misaada mbalimbali kutoka Marekani, UK, Ufaransa, China, Venezuela na jumuia zisizo za serikali kama Red Cross na Islamic Relief zilitangazwa katika vyombo vya habari kuelekea Haiti kusaidia watu waliokumbwa na mtetemeko huo.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©