Sherehe za miaka 46 ya
Mapinduzi ya Zanzibar
14/01/2010

Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Amani Abeid Karume,
akikagua gwaride rasmi la vikosi vya
ulinzi katika kilele cha sherehe za kutimiza miaka 46 ya Mapinduzi ya
Zanzibar katika kiwanja cha Gombani, Pemba, asubuhi ya tarehe 12 Januari
2010.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza
la Mapinduzi Dk. Amani Abeid Karume na Rais Kikwete wakipokea salamu ya
Heshma ya vikosi vya Ulinzi na Usalama wakati wa sherehe za maadhimisho
ya miaka 46 ya Mapinduzi ya Zanzibar zilizofanyika mapema asubuhi ya
tarehe 12 Januari 2010, Gombani, Pemba.

Wananchi walioshiriki katika maandamano ya
kusheherekea miaka 46 ya mapinduzi Zanzibar, wakipita mbele ya Mgeni
rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Amani
Abeid Karume, katika kiwanja cha Gombani, Pemba.

Wananchi wakiwemo Wana CUF na CCM
walijumuika kwa pamoja katika kuadhimisha kilele cha miaka 46 ya
Mapinduzi ya Zanzibar kama ishara wote ni wamoja na wote wanasimama kwa
umoja kwa manufaa ya Zanzibar na Tanzania nzima kwa ujumla.

Kuashiria Zanzibar sasa ni moja na hakuna
tofauti za kisiasa kama ilivyo kuwa hapo awali baina ya CCM na CUF,
wafuasi na wanachama wa CUF walishiriki maadhimisho hayo kwa ukamilifu.
|