Harambee ya mafuriko
Kilosa
15/01/2010

Mlezi wa
Mtandao wa wanataaluma (Tanzania Professionals Network - TPN) Dk. Maua
Daftari (shoto) ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na
Teknolojia, akimkabidhi Katibu Mkuu wa Chama Cha Msalaba Mwekundu (Red
Cross) Tanzania na Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Alhaj Adam Kimbisa,
msaada wa vitu mbali mbali vyenye thamani ya shilingi 1.4m/-
vilivyotolewa na wafadhili baada ya kuhamasishwa na Jamii Forum, Globu
ya Jamii, TPN na mwanakijiji.com kusaidia waathirika wa mafuriko huko
Kilosa katika sherehe fupi iliyofanyika ofisi za Msalaba Mwekundu jijini.
Wengine wanaoshuhudia toka shoto ni Rais wa TPN Mzalendo Sanctus Mtsimbe,
Mike Mushi na Max Melo (wakurugenzi wa Jamii Forum) na Issa Michuzi wa
Globu ya Jamii. Misaada hii ni awamu ya kwanza ya michango hiyo ambayo
bado inaendelea kutolewa.
|