Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Uraia wa Nchi Mbili (Tanzania Diaspora)

20/01/2010

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe akifungua mkutano wa majadiliano baina ya wataalamu wa Tanzania na wa nje ya nchi kuhusu uwezekano wa kuwashirikisha kikamilifu Watanzania walio nje ya nchi. Mkutano huo unaratibiwa na Wizara ya Nje ambayo tayari wameshaunda Idara ya DIASPORA.

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Bernard Membe amesema kuna haja ya kubadili sheria ya uraia ya Tanzania ambayo haimruhusu Mtanzania kuwa na uraia wa nchi mbili kwani sheria hiyo, imepitwa na wakati na haimpi hamasa mtanzania mwenye uraia wan je kuisaidia nchi yake kwa kuwa anakuwa amepoteza uraia wake.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana alisema serikali hivi sasa inalifanyia kazi suala la maombi ya uraia wa nchi mbili na wadau husika wameshaombwa kutoa ushauri.

Alisema kuna haja ya watanzania wanaoishi nje ya nchi kupatiwa uraia wa nchi mbili ili waweze kuchangia na kuwekeza katika rasilimali zilizopo nchini kwa lengo la kuleta maendeleo.

"Tunatumaini kulimaliza suala hili hivi karibuni kwa faida ya wadau wote na taifa letu kwa ujumla," alisema.

Alisema kwa serikali kuruhusu uraia wa nchi mbili kutatoa fursa zaidi kwa wadau kufaidika na haki muhimu ambazo wanatakiwa kupata.

"Kwa kuongeza kipato wakiwa katika mataifa hayo, Watanzania wataweza kuwasaidia wenzao wanaobaki nchini na hivyo kupunguza hali ya umasikini nchini," alisema Waziri Membe.

Membe alisema katika kipindi chote cha uhuru hawakuangalia hilo ila sasa kuna haja kuwashirikisha watanzania wanaoishi nje ili kuleta Tanzania maendeleo.

Alisema wizara ya mambo ya nje imeanzisha idara maalumu ili kujua takwimu za watanzania wanaoishi nje ya nchi kwa kuwatambua kwa vipaji na utaalamu walio nao.

Alisisitiza kuwa watanzania tunaoishi hapa nchini tuwaone wanaoishi nje kama wenzetu na sio kuwatenga pindi watakapopata nafasi ya kupata urai.

Baadhi ya watanzania wanaoishi nje walipata nafasi ya kuchangia katika mkutano huo na kusema kuwa kuna sababu nyingi zinapzowafanya kushindwa kuchangia maendeleo ya nchi yao.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi na Mtaalamu wa nyumba mpya na upangishaji Daniel Mwasandunge ambaye ni mtanzania anayeishi Uingereza alisema kuwa kutokana na nchi kutokuwa na takwimu za wanaoishi nje na taaluma walizonazo imeshindwa kutafuta wataalamu kuanzia wafanyakazi.

"Serikali haina takwimu za watanzania tunaoishi nje na wala haijui taaluma tulizo nazo, hivyo inashindwa kupata wataalamu kuanzia wafanyakazi.

"Tunataka nafasi za ajira zitangazwe kule kama zinavyotangazwa huku kama zipo, kwani tunapofanya kazi tunategemea maisha fulani," alisema Mwasandunge.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©