Dk. Shein atembelea Kilosa
21/01/2010

Hii ndiyo hali halisi ya
Kilosa makazi mengi ya watu bado yamezingirwa na maji shughuli nyingi
bado haziendi vizuri kutokana na athari za mafuriko hayo yaliosababisha
hasara ya uharibifu wa mali na maisha ya watu ambapo kwa sehemu kubwa
wananchi hao wanaishi kwa shida.

Baadhi ya Mitaa ya Mji wa
Kilosa bado imezingirwa na maji kutokana na mafuriko yaliyoikumba wilaya
hiyo na kufanya uharibifu mkubwa wa miundombinu pamoja na mali za
wananchi na kupoteza maisha kwa baadhi ya wananchi.

Makamu wa Rais Dk. Ali
Mohamed Shein akitoka kukagua moja kati ya mahema ambayo yatatumika kama
makazi ya muda kwa wananchi wa Wilaya ya Kilosa katika eneo la Kimamba
alipotembelea Wilaya hiyo kuangalia kiwango cha athari na misaada
inayohitajika.

Makamu wa Rais Dk. Ali
Mohamed Shein akipata maelezo ya ujenzi wa makaazi ya muda toka kwa Mkuu
wa wilaya ya Kilosa Halima Dendegu katika eneo la Magomeni mjini Kilosa
wakati Dk. Shein alipofanya ziara ya kuwatembelea waathirika wa mafuriko
ambayo yameikumba wilaya ya Kilosa kutokana na mto Mkondoa kujaa maji ya
mvua na kina chake kupungua.

Makamu wa Rais Dk Ali
Mohamed Shein akiwafariji baadhi ya waathirika wa Mafuriko yaliyoikumba
wilaya ya Kilosa wakati alipowatembelea katika eneo la Magomeni ambako
inajengwa kambi ya muda ya kuwasitiri wananchi hao ambao kwa sasa
wamehifadhiwa katika ghala la kilichokuwa kiwanda cha mazulia Kilosa.
|