Rais Kikwete awajulia hali
majeruhi wa tukio la ujambazi
22/01/2010

Pichani
Dk. Ramesh Das (shoto) akitoa maelezo ya kitabibu ya Bw. Magambo Sarali
(kitandani) alipotembelewa na Rais Jakaya Kikwete. Bw. Magambo alitoa
ushauri mbele ya Rais kuwa serikali inahitaji kuweka nguvu za ulinzi wa
kutosha kisiwani humo kwa ajili ya usalama kwani kisiwa hicho kina kituo
kimoja ambacho kipo umbali wa kilometa 20.

Inspekta
Mbuma (45), majeruhi wa ajali ya msafara wa Rais iliyotokea juzi wakati
Rais Kikwete akielekea mkoani Shinyanga kukagua miradi mbalimbali ya
maendeleo, amepigwa X ray 3 na kubainika kuwa ana uvimbe kwenye bega,
amepata matibabu na kwa sasa anaendelea vizuri.

Mara
baada ya Rais Kikwete kutia sahihi katika daftari la wageni, ilikuwa
zamu ya Mama Salma Kikwete kama uonavyo pichani akitia sahihi.

Rais
Jakaya Kikwete akiwasalimia baadhi ya Wauguzi wa Hospitali ya rufaa ya
Bugando alipokwenda kuwatembelea kuwaona majeruhi wa tukio la ujambazi
lililotokea katika kisiwa cha Izinga Wilayani Ukerewe, ambapo watu 13
waliuwawa hapo hapo, wakati huo huo watu 10 wakiwemo askari wawili wa
Jeshi la Polisi wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa kuhusika na tukio
hilo la Ujambazi.
|