Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Watanzania waishio UK

23/01/2010

Kamati ya kuandaa mchakato wa upatikanaji wa viongozi wapya wa watanzania hapa Uingereza (taskforce) inawatakia watanzania wote mwaka mpya wenye neema na baraka tele.

Umoja wa watanzania hapa uingereza umekuwa ukifanyiwa tathmini kwa muda ili kuuwezesha kuwa na mwelekeo na mfumo wenye kuleta hamasa, uwazi na ufanisi zaidi katika kutumikia jamii ya watanzania hapa UK.

Kamati kwa ushirikiano na ushauri wa wadau(wanajamii) imeweza kufanya kazi kubwa ya kuleta maono na mwelekeo utakaokuwa na ufanisi zaidi katika kuwatumikia wanajamii wote hapa UK kwa kipindi hiki.

Kamati imeweza kuangalia na Kupendekeza kurekebisha sehemu zote muhimu zilizohitaji marekebisho ili kuleta ufanisi zaidi nazo ni kama zifuatazo:

• Muundo

• Uwakilishi

• Katiba ya Umoja

• Mwelekeo wa Umoja

• Mfumo wa Uongozi wake

Muundo na mwelekeo huu mpya wa umoja wa watanzania utayazingatia mambo ya muhimu ambayo ni muhimu kuyaweka wazi.

• Umoja utahakikisha unaendelea kujifunza; na kuwa wazi katika utendaji wake; kuwaelimisha na kuwawezesha wanajamii wake,ili waweze kuwa sehemu ya mabadiliko na ufanisi katka jamii yetu.

• Mabaadiliko ndio itakuwa changamoto yake: ili kuwa makini kukidhi mahitaji wa wadau wake.

• Umoja utahakikisha unawawezesha wadau ili kuchochea umiliki na uwajibikaji wa wadau katika kuendeleza Umoja wao.

• Utahakikisha unafuatilia, unatambua, kutoa nafasi na unatumia vipaji vyote vilivyo ndani ya watanzania ili kujiendeleza.

• Umoja utahakikisha majukumu ya viongozi(uongozi) yanaainishwa kwa uwazi ili kuondoa miingiliano ya utendaji unaoleta mafarakano; na pia utaweka utaratibu wa kiutendaji utakaokuwa makini kulenga manufaa yawadau wake wakati wote.

Tafadhali watanzania au viongozi wa jumuiya za kitanzania waishio miji ifuatayo, Tunaomba mawasiliano ili tuweze kupata watu watakaokuwa tayari kufacilitate uanzishwaji wa Umoja wa watanzania katika miji yenu.

Cardiff, Milton Keynes, Belfast, Glasgow, Northern Ireland, Norwich, G. Manchester, Portsmouth, Southampton, Leicester, Dublin, Birmingham, Luton Slough, Coventry, London
Scotland, Westmidlands.

Tunaomba muwasiliane na kamati hii ya Umoja wa watanzania kupitia:

Email: Uniting-Communities@yahoogroups.com , au Simu zifuatazo:
Coordinator: 07766168471, Secretary: 07908010344, Members: 07799212095, or 0788841971

Tafadhali anagalia kiambatanisho kwa habari zaidi.

Taarifa ijayo itaambatanisha repoti ya kamati ya taskforce

Asanteni
Umoja wa Watanzania UK

Kwa habari zaidi tafadhali bonyeza hapa.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©