Kikao cha 14 cha Wakuu wa
Afrika
01/02/2010

Rais Jakaya Kikwete (kulia) akisalimiana
na Rais wa Jamhuri ya Libya, Muammar Gaddafi wakati wa kikao cha 14 cha
wakuu wa nchi za Afrika kinachofanyika Addis Ababa nchini Ethiopia
kilichoanza juzi na kutarajiwa kumalizika leo.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsikiliza
kwa makini Rais Omar el Bashir wa Sudan walipokutana kwa faragha katika
siku ya kwanza ya kikao cha 14 cha wakuu wa nchi za Jumuia ya Afrika
kinachofanyika jijini Addis Ababa nchini Ethiopia.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisisitiza
jambo wakati alipokutana na rais Blaise Compaore wa Burkina Faso wakati
wa kikao cha 14 cha wakuu wa Umoja wa Afrika kinachofanyika nchini
Ethiopia.

Rais Jakaya Kikwete akishauriana jambo na
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Mataifa Mheshimiwa
Benard Membe wakati wa kikao cha 14 cha Wakuu wa nchi za Afrika
kinachofanyika Addis Ababa nchini Ethiopia.

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akihutubia
Mkutano Mkuu wa Jumuia ya Wake wa Wakuu wa nchi za Afrika uliofanyika
katika ukumbi wa makao makuu ya Jumuia ya Afrika nchini Ethiopia.
|