Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Jerry Muro kizimbani

05/02/2010

Mtangazaji wa TBC Jerry Muro akisindikizwa kuelekea chemba kusomewa mashitaka ya kula njama ya kutaka kupokea rushwa ya shilingi milioni 10 leo mahakama ya hakimu mkazi kisutu jijini Dar es Salaam.

Jerry Muro chini ya ulinzi mkali mahakamani.

Waandhishi wa habari mbalimbali walikuwapo katika mahakama hiyo akiwamo kaka Michuzi (pili kushoto).

Jerry Muro akiingia ndani ya gari yake huku akipooza koo baada ya kuachiwa kwa dhamana.

Mshtakiwa mwenza na Jerry Muro, Edmund Kapama, akiondoka kwa furaha mahakamani baada ya kuachiwa kwa dhamana leo.

HABARI KAMILI:

Mtangazaji wa TBC Jerry Muro na watu wengine wawili, Edmund Kapama na Deogratius Ngassa, wamepanda kizimbani mchana huu wakikabiliwa na mashataka kadhaa likiwemo la kula njama kutaka kupokea rushwa.

Mbele ya Hakimu Gabriel Mirumbe, Jerry Muro na washtakiwa hao wawili walishtakiwa kwa pamoja kwa kuomba rushwa ya shilingi milioni 10 toka kwa mweka hazina wa wilaya ya Bagamoyo aliefukuzwa kazi hivi karibuni na Waziri Mkuu kwa ubadhirifu Bw. Michael Wage.

Mwendesha Mashtaka wa Serikali Boniface Stancilaus akiwa na Mwendesha Mashtaka toka TAKUKURU Benny Lincolin wamedai mahakamani hapo kwamba mshtakiwa wa kwanza na wa pili pia wanakabiliwa na shtaka la kujipachika wadhifa ambao sio wao.

Inasemekana January 29, 2010 katika hoteli ya Sea Cliff washtakiwa walijitambulisha mbele ya Wage kuwa wao ni maafisa wa Takukuru wakati sio kweli.

Upande wa mashtaka uliiomba mahakama usitoe dhamana hasa kwa washtakiwa wa kwanza na wa pili kwa madai kwamba waliwahi kufungwa huko nyuma na kuwa kwao nje kutaharibu upelelezi ambao haujakamilika na bado unaendelea.

Hakimu alipowataka kutoa uthibitisho kwamba washtakiwa hao waliwahi kufungwa huko nyuma upande wa mashtaka ulishindwa kuthibitisha hivyo dhamana ikawa wazi kwa m ashartia ya kila mmoja kuwa na wadhamini wawili wataosaini bondi ya milioni 5 kila mmoja, ama kwenda rumande hadi Februari 12, mwaka huu kesi itaposomwa tena.

Jerry Muro na Edmund Kapama walitimiza masharti ya dhamana na kuachiwa. Mwenza Ngassa amepelekwa rumande.

Madai ya Jerry Muro na wenzake.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©