Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Mtanange wa Simba na Yanga ughaibuni kufanyika Aprili 4

09/02/2010

Yanga

Mechi ya kwanza ya Simba na Yanga mwaka huu itafanyika Jumapili April 4, kwenye uwanja wa Kalmia, kufuatia mechi itakayochezwa Jumamosi kati ya Stars united na Maryland united japo uwanja itakapochezwa mechi hiyo bado kutangazwa.

Mtayarishaji wa mpambano huo wa Stars na Maryland United, Cyprian, amesema kutakua na nyama choma siku hiyo ya Jumamosi April 3, na mechi hii ni re-union ya wachezaji wote wa Maryland United na kutakuwa na zawadi maalum kwa wachezaji wa zamani wa timu hiyo.

Wachezaji Watanzania waliowahi kuichezea Maryland united ni Liberatus, Mwang'ombe, Vicent Ndusilo, Chiwa Mwombela, Elvis Dotto na Yahaya Kheri. Cyprian ameiomba Stars united wachezaji hao wachezee Maryland united siku hiyo ya mpambano.

Salum Salum amesema yeye hana mkwara wowote, wachezaji hao wanaweza kuchezea timu hiyo, lakini wajue hawatakiwi kuifunga timu yao, mchezaji yeyote atakaeifunga timu yake ya Stars United ajue amefungiwa, wewe cheza tu lakini ujue unatoa pasi tu.

Simba

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©