Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Gari yaacha barabara na kupanda mti

11/02/2010

Gari lenye namba za usajili T 857 BAR, likiwa limening’inia juu ya mti katika daraja la Kawe lililopo Mbezi kwa Komba, Dar es Salaam.

Haikuweza kufahamika chanzo cha ajali ya gari hilo, kwa mujibu wa walioshuhudia ajali hiyo walieleza kuwa ajali hiyo ilitokea saa tisa usiku.

Huu ni upande wa chini ya gari hilo linavyoonekana likiwa juu ya mti, ambapo imeelezwa magari kadhaa yalifika kutoa huduma ya kuliondoa mahala hapo bila mafanikio.

Askari wa usalama barabarani, akiongoza magari ili kuondoa foleni ambayo ilikuwa ikisababishwa na madereva waliokuwa wakishangaa ajali hiyo jambo ambalo lilifanya kila dereva kupunguza mwendo afikapo eneo hilo.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©