Daraja la Vingunguti
05/05/2010

Daraja
la Vingunguti lililokuwa njia mbadala ya magari kutoka Tabata kuingia
Vingunguti Kiembe Mbuzi kuvuka mto Msimbazi limejengwa hivi karibuni kwa
gharama ya mabilioni ya shilingi, hivi sasa daraja hilo limevunjika
baada ya mvua ya msimu mmoja tu iliyonyesha jijini Dar es Salaam.

Jiji
la Dar es Salaam lina madaraja mengi, na mengi ya madaraja hayo huweza
kustahimili mvua ndiyo maana yanaendelea kutumika nyakati zote. Mpaka
sasa haijajulikana ni kipi hasa kilichosababisha daraja hili la
Vingunguti liharibike haraka?
|