Abu Dhabi yaweka machine
inayotema Dhahabu (ATM)
13/05/2010

Tumeshaona mashine za
kutoa pesa, vinywaji, vitafunio, vyakula, na kadhalika... Hoteli ya
Emirates Palace iliyopo Abu Dhabi imekuwa ni hoteli ya kwanza duniani
kuweka mashine ya namna hiyo ambayo badala yake inatoa Dhahabu baada ya
kulipa pesa kamili inayotathmini thamani ya dhahabu ya wakati uliopo.

Hoteli ya ya Emirates
Palace iliyojengwa kwa dola bilioni tatu ($3bn)ambayo inamilikiwa na
serikali, imeonakana ni sehemu muwafaka ya kuwekwa mashine hiyo 'Gold To
Go' ambayo yenyewe imetengenezwa na kupambwa kwa dhahabu yenye thamani
ya 24-carat.
|