Meya wa Mwanza ahojiwa juu
ya mauaji ya Bi Bahati
20/05/2010

Kufuatia mauaji ya utata ya Bi Bahati Stephano yaliyotukia jijini Mwanza,
Kamanda wa polisi jijini humo bwana Simon Siro amesema, "...Jana jioni
majira ya saa kumi pale Uwanja wa Ndege wa Mwanza tuliweza kumkamata
mheshimiwa Leonard Bandiho Bihondo (pichani juu) ambaye ni mstahiki Meya
wa jiji la Mwanza ana umri wa miaka 64 kwa tuhuma hii ya mauaji ya Bi
Bahati Stephano aliyekuwa katibu wa CCM Isamilo jijini Mwanza.

Hii
imekuja mara baada ya kufanya mahojiano na watuhumiwa wote watatu ambao
tayari tumekwisha wakamata, wote wamekuwa wakimtaja kwamba ndiye
anayehusika katika tukio hili. Kwa hiyo, mahojiano yanafanyika ili
tuweze kujua ukweli wa tuhuma hizi na kama tutathibitisha bila mashaka
kwamba anahusika na mauaji haya aidha kwa kula njama au kwa, au kwa njia
nyingine basi tutampeleka mahakamani na sheria kuchukua mkondo wake.
Lakini niombe kwamba bado tunahitaji taarifa nyingine nyingi maana
tunajua suala la kesi ya mauaji ni kubwa na linahitaji ushahidi ulio
mkamilifu toka pande zote mbili kwa lengo la kuhakikisha kwamba
hatutomwonea mtu yeyote ili kulinda haki ya kila mtu na kuhakikisha
kwamba hakuna mtu aliyeko juu ya sheria."
|