ATCL yaachisha
wafanyakazi
27/05/2010

Kamati
ya kudumu ya Bunge na Fedha na Uchumi iliyokutana jijini Dar es Salaam
tarehe 25 Mei 2010 imeridhia mapendekezo na ushauri wa Ofisi ya Msajili
wa Hazina la kuwaachisha kazi Wafanyakazi wote wa Shirika la Ndege
Tanzania (ATCL) ili kuipunguzia mzigo Serikali. Ushauri huo umetolewa na
mshauri wa Msajili wa Hazina bwana Godfrey Msella kwa kusema, "kama ATCL
haibebeki, ni bora Serikali ibwage manyanga" na hivyo kufuatiwa na tamko
rasmi la Mwenyekiti wa tume hiyo ya Bunge, mhe. Abdallah Kigoda.
Hatua kama hiyo iliwahi kuchukuliwa katika shirika la Bima la Taifa
(NIC) na imependekezwa kuwa hatua hii isiishie ATCL pekee bali ifike pia
katika Shirika la Reli nchini (TRL).
|