Wahamiaji 21 kinyume na
sheria watiwa mbaroni Tumbatu
04/06/2010

Jumla ya wahamiaji haramu 21 wamekamatwa
baada ya kuingia nchini kinyume cha sheria na Idara ya uhamiaji Zanzibar
kwa kushirikiana na Kikosi cha Kuzuwia Magendo KMKM katika Maeneo ya
Tumbatu Unguja.
Katika taarifa yake Afisa Uhusiano wa Idara hiyo Muhsin Abdalla Muhsin
amekiri kukamatwa kwa watu hao wakiwa ni raia wa Kenya ,Somali na
Ethiopia ambao wameingia nchini kinyume cha sheria.
Amesema wamepata taarifa ya kukamatwa kwa watu hao siku ya Jumamosi na
kikosi cha KMKM kwa msaada wa wananchi kutoa taarifa ya uwepo kwa watu
hao .
Hata hivyo watuhumiwa hao wamefikishwa mahakamani kwa ajili ya hatua
zaidi za kisheria.
Aidha amewataka wananchi kutoa taarifa zaidi ambapo wanagundua kuwepo
kwa wageni ambao wanawatilia mashaka ili hatua za kiusalama ziweze
kuchukuliwa.
|