Mechi ya Taifa Stars na
Brazil kutoonyeshwa TV za majumbani
05/06/2010

Katibu Mkuu wa Shirikisho la soka Tanzania
(TFF) Frederick Mwakalebela akizungumza na waandishi wa habari jijini
Dar es Salaam katika ukumbi wa Habari-Maelezo amesema kuwa mechi ya
kirafiki kati ya Taifa Stars na Brazil haitaoneshwa moja kwa moja (LIVE)
na runinga za nyumbani Tanzania bali vituo hivyo vya luninga
vitaruhusiwa kurusha mechi hiyo mara baada ya dakika 90 za mchezo.
|