Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Taifa Stars na Brazil uwanjani

07/06/2010

Mechi iliyochezwa siku ya Jumatano nchini Zimbabwe kati ya timu ya mpira wa miguu ya Taifa ya Brazili na ile ya Zimbabwe imeweza kuiingizia nchi hiyo jumla ya dola za Kimarekani laki sita (US$600 000) kutoka kwa watu wapatao elfu hamsini waliolipia ili kuweza kuiona mechi hiyo.

Kwa mujibu wa waandaaji wa mechi hiyo, Mamlaka ya Utalii ya nchini Zimbabwe -- Zimbabwe Tourism Authority (ZTA)-- baadhi ya fedha bado zinaendelaa kukusanywa kutoka katika makampuni ambayo yalinunua tiketi hizo kwa ajili ya wafanyakazi wao walioketi katika viti vya watu maarufu na wale maafuru sana (VVIP and VIP).

Waandaaji hao wanasema kuwa walitoa tiketi za bure (complimentary tickets) kwa mabalozi mbalimbali na makampuni kadhaa ila cha kushangaza ni kuwa, tiketi hizo za bure ziliuzwa kinyemela na watu kuingia nazo kiwanjani na hivyo kuwasababishia waandaaji hao kukosa mapato ya tiketi hizo. Kituo cha radio cha VOP kinaripoti kuwa kilifanikiwa kuiona tiketi ya VVIP ikiuzwa kinyemela nje ya Uwanja.

Vijana wa timu ya Taifa ya Zimbabwe, Samba Boys, walilipwa kitita cha jumla ya dola milioni 2.5 kwa ajili ya kucheza mchezo huo.

Serikali imefikia asilimia 45% ya gharama ilizotumia katika mechi hiyo wakati kwa upande wa makampuni, wengi wao hali haikuwa kama walivyotarajia kwani timu ya taifa ya Brazili ilichukua nafazi zote za matangazo katika mechi hiyo. Wachuuzi wadogo wadogo nao wamefurahia ujio wa Brazili kwani waliripoti ongezeko la kipato kutoka kwenye biashara zao walizozianza tangu asubuhi katika maeneo ya kiwanja hicho.

Mchezaji mashuhuri wa Brazili, Kaka aliwafurahisha watazamaji waliofika kiwanjani mara baada ya kipenga cha mwisho kulia, kwa kuwarushia jezi yake "sandakalawe" kwa ajili ya kumbukumbu kwa atakayeipata, nao wachezaji wa Zimbabwe walifanya hivyo.

Timu ya Brazili itashuka katika kiwanja cha mpira wa miguu cha Taifa ili kucheza na timu ya Tanzania, Taifa Stars. Tiketi kwa ajili ya mechi hiyo zimekuwa zikiuzwa na TFF kwa kati ya dola 25 hadi 180 kutegemea na watakakoketi watazamaji. Inasemekana kuwa TFF wamelipa kiasi cha dola za Kimarekani milioni 2.5 kwa Brazili kwa ajili ya kuipata mechi hiyo.

 
   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©