Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Brazil 5 Tanzania 1

08/06/2010

Heka heka langoni

Mpira umetinga wavuni

Kipa anajizoa chini

Shangwe na manyago golini. Picha na Issa Michuzi

Habari Kamili

Aliyeongoza kufungua kitabu cha magoli ni Robinho aliyeifungia timu yake bao kunako dakika ya 10. Ilimchukua tena Robinho takriban dakika ishirini hivi ambapo dakiak ya 33 aliiandikia timu yake bao la pili ambalo lilidumu hadi kipindi cha kwanza kumalizika.

Kipindi cha pili kilianza na mnamo dakika ya 52 mchezaji wa Brazili Ramires, aliifungia timu yake bao la tatu. Mchezaji machachari wa Brazili, Kaka, ambaye kwa takriban mwaka mmoja alikuwa hajaifungia bao lolote timu yake ya taifa alifanikiwa kufuta nuksi hiyo pale alipachika bao katika dakika ya 75 ya mchezo.

Ilikuwa ni mchezaji Aziz aliyeusindikiza vyema mpira uliochongwa kutoka kwenye kona na hivyo kuipa Tanzania kifutia machozi kunako dakika ya 85 ya mchezo.

Ndani ya dakika tatu za majeruhi, zikiwa zimesalia dakika mbili na ushee, ilikuwa ni Ramires aliyeamua kuonesha kuwa 'alikuwepo' kwa kupachika bao lake la pili na la 5 kwa timu yake ya Brazil.

Hivyo hadi kipenga cha mwisho kinali, ni Brazil 5 Tanzania 1.

Mrisho Ngassa aling'ara katika muda wote aliocheza lakini jitihada zake ziliishia mikononi mwa kipa wa Brazili au kutolewa nje. Mchezaji Jerson "Jerry" Tegete aliingia dakika chache kabla ya mechi kwisha na kuchukua nafasi ya Ngassa lakini naye hakufanikiwa kupata goli.

Timu ya Brazili ilishusha nyota wake ambao wanaunda kikosi kitakachoshiriki katika michuano ya kuwania kombe la Dunia kwa mchezo wa soka.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©