Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Aliyemkubatia KAKA katika mechi ya Tanzania na Brazil

12/06/2010

Kijana Nagery Ally Kondo (pichani juu) alifika katika studio za redio Clouds FM na kuhojiwa katika kipindi cha Power Breakfast Juni 10, 2010 na Dina Marios anaandika hivi katika blogu yake "...wakati wanaenda uwanja wa taifa yeye na wenzake walikata tiketi ya Tsh 30,000 lakini kutokana na kutokuwa na watu Maaskari waliwaruhusu kukaa jukwaa la Tsh 80,000....mpira ulipokolea Washikaji zake walimuona jamaa anavua mkanda, saa, viatu akawaomba wamshikie simu na kuwaambia mie naenda hivyo kumkumbatia Kaka. Wenzie walijua utani mara jamaa akaanza kukimbia akielekea uanjani na kwenda kumkumbatia Kaka.Na anasema wakati anaenda alikuwa anajua lazima yatampata makubwa lakini alishaamua potelea mbali Mzuka wa soka ushampanda liwalo na liwe.

Anasema hakupanga chochote toka anatoka nyumbani mzuka ulimpanda wakati anaangalia soka hapo uwanjani na akajikuta anatamani kwenda kumkumbatia Kaka na ndicho alichofanya." -  Dina Marios.

Watu kadhaa wametoa hisia mchanganyiko kuhusiana na tukio hili. Baadhi wamesema kuwa kwa kuwa alikuwa na nia njema na kwa kuwa kitendo kama hiki hutokea kwingineko duniani, basi adhabu yake isiwe ya kutisha. Wapo waliohoji umakini wa askari katiak kazi yao kuhusiana na hili. Vile vile wapo waliasa kuwa endapo kijana huyu angekuwa ameficha silaha na kumdhuru yeyote kiwanjani, ingechafua kabisa nchi ya Tanzania na hili laweza kutokea kwani mtu anaweza kuficha silaha popote na kuitumia haraka.

Nagery Ally Kondo akijitosa uwanjani...

Kwa raha zake...

Lengo lake ni kumkumbatia KAKA tu...

Hatimaye azma yake imetimia, KAKA bia ajizi amkumbatia Ally Kondo...

Sasa lengo limetimia ni wakati wa kuondoka mechi iendelee...

mkono kwa mkono, bega kwa bega...

Haya sasa nenda bwana Kondo tuendelee na boli...

Oyeee! nimetimiza azma yangu...

Kwa heri bwana Kondo...

Shadarack Nsajigwa (namba 14) kapteni wa Taifa Stars akishangaa jamaa aliyejitosa kwenda katikati ya uwanja kumkumbatia KAKA wakati mechi inaendelea...

Ya mwisho mwishooo...

Kwaherini...

Sasa nipelekeni kokote sina neno, azma yangu nishaitimiza...

Sijapata kufurahi maishani mwangu kama leo...

Twende zetu huku tukazungumze kwa kituo...

Kijana wetu huyu hana tatizo huyu, ni mshabiki tu kama mashabiki wengine, lakini tunaye...

Nagery Ally Kondo (21) akiwa ndani ya ofisi za Clouds FM Radio katika kipindi cha 'Power Breakfast' na Gerald Hando (shati jekundu) na Paul James (PJ) mwenye kofia.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©