Matayarisho ya Sabasaba
2010
13/06/2010

Hili ndilo Bango la
matangazo linaloonekana katika geti kuu la kuingilia katika Viwanja vya
Mwalimu Nyerere, kwenye maonyesho ya Sabasaba 2010.

Mafundi wakiwa katika
shughuli za ujenzi na ukarabati wa sehemu za viwanja hivyo ili kuweka
sawa kabla ya kuanza maonyesho hayo yanayotarajia kuanza Julai mosi
mwaka huu.

Hawa pia ni mafundi
wakikokota mbao zao kwa ajili ya kwenda kujengea vibanda ndani ya
viwanja hivyo.

Wafanyakazi wa
kukodishwa katika ujenzi na ukarabati wa mabanda ya Maonyesho ya Saba
Saba wakiendelea na ujenzi ndani ya Viwanja vya Mwalimu Nyerere Dar es
Salaam ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Maonyesho hayo yanayotarajia
kuanzanza Julai 1 mwaka huu.

Katika kazi hakuna
kuremba, hata kina mama wameweza kujitokeza kwa wingi katika viwanja
hivyo na kushirikiana na mafundi wa kiume katika ujenzi na ukarabati na
wengi wao wamekuwa wakibeba zege na mchana viwanjani humo ni ilimradi tu
mkono uende kinywani siku hizi wanawake pia hawachagui kazi hivyo ukiwa
na kazi yoyote usisite kumshirikisha mwanamama kwa kuhofia anaweza
kukataa, ila iwe kazi halali.

Haya ni mabanda
yaliyotumiwa na Wizara ya Afya katika maonyesho ya mwaka jana, ambayo
pia yako katika hali nzuri baada ya kufanyiwa ukarabati wa hali ya juu
na wa kupendeza kama yanavyoonekana.
|