Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Polisi wakamata madawa ya kulevya

24/06/2010

Kamanda wa Kikosi cha Madawa ya kulevya, Godfrey Nzowa, mbele ya Waandishi wa habari kwenye Ofisi za makao Makuu ya Polisi jijini Dar es Salaam  ameonesha mifuko na madawa ya kulevya yaliyokamatwa kutoka kwa watuhumiwa Diaka Brama Kara (52) raia wa Guniea-Conakry na Abubakar Ndijane (50) raia wa Liberia.

Madawa ya kulevya yaliyokamatwa ni  aina ya Cocaine yanayokadiriwa kuwa na uzito wa kilogramu 31. Madawa hayo yalikamatwa wakati watuhumiwa walipofika katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere tarehe 23 Juni 2010 wakitokea nchini Afrika ya Kusini na ndege namba SA 199.

Watuhumiwa hao walikuwa wamebeba mabegi yenye nembo za  kidiplomasia (Diplomatic Bag) ili kupunguza uwezekano wa kutokukaguliwa lakini askari waliwashuku na walipohojiwa walidai kuwa wao ni wanadiplomasia wanatoka Ubalozini, pamoja na majibu hayo, askari waliwatia mashaka na hivyo kuamua kuwapekua na kuwakuta na madawa hayo. Watuhumiwa wapo mahabusu kwa upelelezi zaidi.

credit: Muhidin Sufiani/sufiani mafoto blog na Baraka Mfunguo/mtwara kumekucha blog

YATOKANAYO
Madhara ya matumizi holela ya madawa ya kulevya ni makubwa na yamezidhuru jamii zote duniani. Familia nyingi zimeparaganyika kutokana na madhara haya. Ni jukumu la wananchi kupambana ili kuzuia madhara ambayo yanaathiri hata wale wasiohusika moja kwa moja kwa mfano, wizi na udokozi wa vitu na kuviuza ili kupata fedha ya kununulia madawa ya kulevya ili kukidhi haja ya mwili. Wapo wazazi, wazee na watoto ambao wameumizwa na vijana wanaotumia madawa ya kulevya. Pia, zipo familia zilizogombana, zilizotengana na hata watu kufa kwa sababu ya athari ya biashara au matumizi ya madawa ya kulevya.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©