Tapeli akamatwa na
Mwanamama
27/06/2010

Pichani wanaonekana wakazi na
wafanyabiashara wa eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam wakimshangaa
mwanamke ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja akiwa
anamdhibiti tapeli wa mchezo wa bahati nasibu.

Kijana huyo mwenye shati jeupe anayedaiwa
kujifanya ni muwakilishi wa kampuni ya bahati nasibu kwa kutumia watu
SMS za ushindi na kuwataka kutuma fedha ili wapate zaidi.

Mama huyo aliweka mtego baada ya kutuma
fedha ambapo tapeli huyu anadaiwa kumtaka mhusika apeleke shilingi laki
mbili eneo hilo ili awekewe milioni moja katika simu yake.

Ndipo Mwanamke huyo alipomnasa tapeli huyo.

Mguu kwa mguu akimuwelekeza polisi.

Mwanamama akiwasili na tapeli huyo polisi
kumfungulia mashtaka yake.
|