Ajali ya Ngalawa Dar es
Salaam
28/06/2010

litokea ajali ya boti ya Seagull kuigonga
ngalawa iliyokuwa ikipita karibu yake. Waliokuwa kwenye ngalawa
waliokolewa japo chombo chenyewe kilizama majini. Haijaripotiwa kupotea
uhai kwa yeyote katika ajali hiyo.

Watu 11 wamenusurika kufa maji, baada ya
ngalawa yenye jila la Usilolijua, kugongana na boti ya Kampuni ya Sea
Gull, ya Zanzibar. Ajali hiyo iliyohusisha jahazi linalofanya biashara
ya kusafirisha vinywaji aina ya bia na bidhaa nyingine kutoka Dar es
Salaam kwenda Zanzibar, ilitokea saa 7:00 mchana. Hata hivyo wakati
ajali hiyo inatokea, jahazi lilikuwa na kreti tupu 1,400 za bia na
ilikuwa inakuja Dar es Salaam kubeba bia.

Nahodha mkuu wa jahazi, Musa Machano (35), alisema wamepoteza kreti zote,
nguo, viatu, simu na fedha taslimu Sh180,000 baada ya jahazi kugongwa
wakati wanakaribia kufika eneo la kutia nanga. Machano alisema kabla ya
tukio hilo, alishaonyesha ishara ya bendera kwa nahodha wa boti ya Sea
Gull kuashiria kuwa alikuwa katika eneo hilo na kwa hiyo apunguze mwendo
na kubadili njia, lakini haikusaidia.

"Nilimuonyesha nahodha mwenzangu ishara kwamba niko eneo lile, lakini
haikusaidia kwa sababu aliendelea kuja kwa mwendo ule ule aliokuwa nao
na kunigonga sehemu ya ubavuni upande wa kulia,"alisema Machano. "Tunawashukuru
wenzetu kwa msaaada waliotupa kwani bila wao kile kitambaa kilichokuwa
kimetufunika kingeweza kutusababishaia vifo," alisema. "Hii jahazi yetu
inategemea upepo si kama boti ya mwenzetu inayotumia mashine.
Nilipomuonyesha ishara mwenzangu alitakiwa kunikwepa na kupita sehemu
nyingine lakini badala yake alitugonga kwa makusudi,"alisema Machano.
Alisema ndani ya jahazi kulikuwa watu 11.
Aliwataja wenzake waliokuwemo kwenye jahazi hilo kuwa ni, Kaimu Amri
(50)Musa Machano(35)Hamis Abdalah(18)Hamis Makame(14) Nasoro
Muhamed(15). Wengine ni Rashd Fumo(15), Hamis Shauri(24),Haji Sahaban
(22) na mmoja aliyetambulika kwa jina moja la Mati (32).
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar
es Salaam, Suleiman Kova, alifika katika eneo la tukio na kuzungumza na
watu walionusurika na kuahidi kuwanunulia simu kwa kila mmoja, baada ya
simu zao kuzama majini. "Wakati tunaendelea kuwasiliana na Mamlaka ya
Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) kuangalia sheria za
ajali ya majini zinasemaje kila mmoja nitampa simu nyingine,"alisema
Kova.
|