Mama Salma azindua
ukarabati sekondari Tabora
29/06/2010

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete amezindua
rasmi awamu ya kwanza ya ukarabati na upanuzi (Rehabilitation and
Extension) wa shule ya sekondari ya wasichana ya Tabora unaofanywa kwa
hisani ya Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) kwa gharama
ya zaidi ya shilingi bilioni 1.7. Waliohudhuria uzinduzi huo ni
wanafunzi wa shule za Tabora Wasichana, Tabora Wavulana na Mirambo
pamoja na walimu na Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Abeid Mwinyimsa.

Mke
wa Rais, Mama Salma Kikwete, akiwahutubia wanafunzi wa shule za
Sekondari za Mkoa wa Tabora wavulana na wasichana na Mirambo wakati wa
sherehe za uzinduzi wa upanuzi na ukarabati wa shule ya sekondari Tabora
wasichana uliofanyika jana mkoani humo.

Mama Salma Kikwete
akitembelea moja ya bweni lililokarabatiwa katika shule ya wasichana ya
Tabora baada ya kuzindua mradi wa ukarabati na upanuzi wa shule hiyo.
|