Ndege yaanguka Tanga
30/06/2010

Kwa mujibu wa taarifa ya habari ya mchana
kupitia TBC1, ndege ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) ya kituo cha
Ngerengere mkoani Morogoro imeanguka katika eneo la Manga-Kabuku mkoani
Tanga.
Ndege hiyo ilikuwa katika mazoezi na
ilipata hitilafu hivyo ikabidi kutua kwa dharura katika barabara na
hivyo kusabisha kugongana uso kwa uso na basi lililokuwa limebeba
watalii lililokuwa katika eneo hilo la barabara.

Ndege hiyo ilikuwa imebeba watu watatu ambapo wawili walikuwa ni
marubani na mmoja wao alifariki papo hapo. Imeripotiwa kuwa hakuna
abiria yeyote katika basi la utalii aliyepoteza uhai.
Ndege hiyo imesababisha barabara isipitike
na hivyo kukwamisha usafiri kwa abiria wanaotoka na kuingia kwa kutumia
barabara inayounganishwa na mikoa ya Kaskazini na ile inayounganishwa na
mkoa wa Pwani.
|