Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Ndege iliyonusurika kuanguka Zanzibar

06/10/2010

Mwishoni mwa wiki, ndege ndogo ilibidi kutua kwa dharura barabarania baada ya kupata hitilafu ya mashine yake eneo la Chau nje kidogo ya kijiji cha Mtende, Makunduchi wilayani Kusini Unguja.

Meneja Mawasiliano ya Anga Zanzibar, Said Sumry, alisema ndege hiyo inayomilikiwa na kampuni ya Tropical Air, ilikuwa ikitumika kwa mafunzo ya urubani ambapo rubani Keyvan Cazdat, raia wa Iran, alikuwa akimfundisha urubani, Abrahman Mohammed, raia wa Tanzania.

Ndege hiyo iliruka katika Uwanja wa Ndege wa Zanzibar, Kiembesamaki nje kidogo ya mji wa Zanzibar, siky ya Ijumaa, Oktoba Mosi majira ya saa 3.44 asubuhi, na ilipofika eneo hilo saa 3.55, ilipata hitilafu ikiwa angani, ndipo rubani  akaamua kutua barabarani.  Rubani huyo na mwanafunzi wake walisalimika ingawa ndege ilipata athari kidogo kutokana na kuingia kwenye msingi wenye mawe.

Sumry alisema ndege hiyo yenye namba 5H-TFS aina ya Piper 28-140, kwa kawaida hutumika kuwapa mazoezi marubani wanafunzi katika eneo hilo, kutokana na kutotumiwa na ndege nyingine.

Hili ni tukio la pili kwa mwaka huu kwa ndege kutua barabarani kwa dharura. Mapema mwaka huu, ndege ndogo kama hiyo ilitua katika barabara ya Kiwengwa mkoa wa Kaskazini Unguja.  Miaka kadhaa iliyopita, ndege ndogo ya kampuni hiyo ya Tropical Air iliwahi kuanguka baharini karibu na kisiwa cha Chumbe, wilaya ya Kusini Unguja, ikiwa na abiria wawili, mtu na mkewe.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©