Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

TIGO yaikabidhi S/M Sinza basi jipya

07/10/2010

Kampuni ya simu za mkononi Tigo imekabidhi basi jipya aina ya TATA lenye thamani ya dola $ 71,250 ambazo zinakadiriwa kuwa zaidi ya shilingi milioni mia moja na sita.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Afisa Mjasiliamali Watu Tigo Benneth Kakorozya alisema “ kampuni yetu leo imejitolea kununua Gari jipya (basi) litakalotumika kwa shughuli za kusafirisha wanafunzi wa shule ya Serikali ya Sinza Maalum iliyopo chini ya Manispaa na Wizara ya Elimu pia TAMISEMI.

Tumeona mahitaji ya shule hii ya sinza maalum, walikuwa na gari bovu hali iliyopelekea hata wanafunzi wengi kutohudhuria shule kutokana na kukosa usafiri na hatimae kuacha shule kabisa Tigo tumeliona hilo na limetugusa hivyo tukaona ni vyema kukabiliana nalo leo.

Lakini pia Dhumuni letu ni kuuunga mkono jitihada za serikali chini ya Wizara ya Elimu katika kuendelea kukuza kiwango cha elimu nchini kwa kuziwezesha ngazi mbalimbali tukianzia na shule za msingi kwa kupambana na changamoto zinazokabili sekta hii.

Leo hii Tigo tunajisikia fahari sana kutoa mchango wetu huu kusaidia wanafunzi ambao tunaamini ndio taifa la kesho.

Mheshimiwa Naibu Katibu mkuu Wizara ya elimu na Mafunzo ya Ufunzo ya Ufundi, Tigo tunachukua nafasi hii kukufahamisha rasmi kuwa makabidhiano ya Basi hili ni muendelezo wa mikakati madhubuti tuliyopanga tangu awali ya kuhakikisha tunasaidia jamii tunayoihudumia kwenye biashara yetu.

Tigo tunatambua sana umuhimu wa wateja wetu hivyo tumejikita kusaidia jamii kwenye swala la Elimu, Afya, Mazingira, Kampuni ya Simu za mkononi Tigo imekua ikisaidia jamii kwenye sekta ya mawasiliano kwa kutoa huduma bora kwa kuzingatia zaidi unafuu wa huduma kuliko mtandao wowote nchini.

Pia katika elimu ya jamii na afya mwezi uliopita tu Tigo imechangia zaidi ya shilingi milioni 76 kwa hospitali ya CCBRT kuchangia mradi wa kupima na kutibu macho bure utakaoanza kufanyika kule Mwanza mwezi huu na pia kufundisha wakunga jinsi ya kuhudumia jamii kwa hospitali mbalimbali.

Kwaniaba ya Tigo ninaomba nitangulize shukrani zangu kwa wewe kukubali kutenga muda kwaajili ya kuungana nasi katika tukio hili la kijamii na la kihistoria ili kuboresha elimu nchini.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©