Timu ya
Taifa ya Morocco imeweza kujipatia
pointi kwa goli la ugenini baada ya
kuifunga timu ya Taifa ya Tanzania,
Taifa Stars, bao moja kwa bila.
Mchezaji
wa Morocco, mshambuliaji Mounir El-Hamdaou
ndiye aliyefunga bao hilo pekee la
mchezo kwa shuti kali toka mguu wa
kushoto, lililomshinda mlinda mlango
Juma Kaseja, dakika mbili tu kabla ya
kumalizika kwa kipindi cha kwanza na
kwenda mapumziko mafupi.
Mchezo huo
ulifanyika katika uwanja wa Taifa jijini
Dar Es Salaam.