Wachimba
migodi 33 walionaswa chini ya ardhi
yapata urefu wa mita 700 kwenda chini
(futi 2,300) kwa zaidi ya miezi miwili
katika machibo ya mgodi wa San Jose
karibu na Copiapo, nchini Chile,
hatimaye wapatiwa ufumbuzi wa kuokolewa.

Wachimba
migodi hao walikuwa wakihudumiwa kwa
virutubisho maalumu vya afya vilivyokuwa
vikipenyezwa katika upenyo uliochimbwa
kwenye maeneo ya mgodi na kuwafikia.
Waliweza pia kuwasiliana na jamaa zao
kwa njia ya mawasiliano ya video.

Wachimbaji
wote 33 waliokolewa salama na
wataendelea kupatiwa huduma muhimu.
