Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Huduma ya afya ya bure kwa wakazi wa Dar es Salaam

16/10/2010

Wakazi wa Dar es Salaam wanatarajiwa kupata huduma za kinga na tiba kutoka meli maalumu ya tiba ya Jeshi la China ambayo itapiga nanga Oktoba 19, mwaka huu.

Meli hiyo yenye madaktari na wauguzi takribani 428 itatoa huduma hizo bure. Akizungumza na waandishi wa habari Jijini leo, Balozi wa China nchini Tanzania, Liu Xinsheng alisema, huduma hizo zinatarajiwa kutolewa kwa siku tatu kuanzia Oktoba 20, 21 na 22.

“Tunawataka wananchi wenye matatizo mbalimbali kujitokeza katika meli hiyo na kupatiwa matibabu kwa matatizo mbalimbali yanayowasumbua,“ alisema Xinsheng.

Alisema meli hiyo itatoa huduma za vipimo, ushauri, tiba ya asili kutoka China pamoja na tiba ya kisasa na upasuaji mkubwa na mdogo.

Alisema meli hiyo inayoitwa ‘Ark Peace’ ina vitanda 500 na vyumba vya upasuaji vinane kwa ajili ya kutoa huduma ya kulaza wagonjwa watakaoonekana kuwa wanahitajika kupewa huduma hiyo na kwamba huduma zote zitafanyika ndani ya meli.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©