Rais Karume alisema kuwa
umuhimu wa kujenga afisi
hizo unakuja kutokana na
kuongezeka haja na
shughuli za afisi hizo,
katika kuimarisha
utekelezaji wa kazi na
mambo ya Muungano.
Katika hotuba yake, Rais
Karume aliipongeza afisi
ya Makamu wa Rais chini
ya uongozi wa Dk. Ali
Mohammed Shein, kwa
kujenga jengo hilo la
kisasa hapa Zanzibar,
ambalo ni kielelezo cha
mapenzi yao kwa
Zanzibar.
Aidha, Dk. Karume
alimpongeza na
kumshukuru aliyekuwa
Gavana wa Benki Kuu ya
Tanzania (BOT), marehemu
Daud Balali kwa uwamuzi
wake wa kujenga afisi ya
kisasa ya taasisi hiyo
hapa Zanzibar.
Mbali ya kusifia usanifu
na ujenzi wa jengo hilo,
Dk. Karume alihimiza
utunzaji wa majengo hayo
na kueleza umuhimu wa
kutengwa bajeti maalum
ya matunzo na
uendelezaji wake.
Akizungumzia ujenzi wa
afisi na makaazi hayo,
Katibu Mkuu afisi ya
Makamu wa Rais, Ruth
Mollel, amesema kuwa
ujwenzi huo umegharimu
zaidi ya shilingi za
Tanzania, bilioni 10.3,
ambapo zaidi ya bilioni
8.6 ni kwa ujenzi na
zaidi ya bilioni 1.7 ni
za utaalamu.
Mollel alieleza
kuwa ujenzi huo
ulioanza Julai
2007 na
kumalizika mwaka
huu, umefanywa
chini ya
Ukandarasia wa
Kampuni ya
Railway
Chianchang
Engineering ya
China na
kusimamiwa na
Chuo Kikuu cha
Ardhi cha Dar-es-Salaam.
Aidha, Katibu
Mkuu huyo alitoa
shukurani kwa
Serikali ya
Mapinduzi
Zanzibar chini
ya uongozi wa
Rais Karume kwa
kupewa eneo hilo
kwa ajili ya
ujenzi huo wa
afisi na nyumba
ya makaazi ya
Makamu wa Rais.
Nae Waziru wa
Nchi Afisi ya
Makamu wa Rais (Muungano),
Mohammed Seif
Khatib, alisema
ujenzi wa afisi
hiyo ni
muendelezo wa
hatua za
Serikali ya
Jamhuri ya
Muungano wa
Tanzania kujenga
afisi zake za
kudumu hapa
Zanzibar.
Alizitaja
miongoni mwa
afisi hizo kuwa
ni Afisi ya
Uhamiaji Mkoa wa
Kusini Unguja,
jengo jipya
linalojengwa la
Afisi Kuu ya
Uhamiaji
Zanzibar, jengo
jipya la afisi
ya Bunge, nyumba
ya kulala wageni
huko Madungu
Pemba na jengo
la Benki Kuu
lililopo Gulioni
mjini Zanzibar.