Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Balozi Mwanaidi katika maonyesho Marekani

24/10/2010

Mwana blogu Mubelwa Bandio alihudhuria uzinduzi wa blogu ya http://lukemusicfactory.blogspot.com ambapo anasema, ilikuwa nii zaidi ya uzinduzi...., Ni zaidi ya maonesho.... yaani, ni mjumuiko wa Watanzania na utambulisho wa ujasiriamali wa Watanzania, kwa Watanzania.

Mheshimiwa Balozi akipokelewa na waandaaji wa uzinduzi huo Usiku wa kuamkia leo, uliofanyika katika ukumbi wa Mirage Hall mjini Hyattsville, jimbo la Maryland Marekani.

Blogu ya Vijimambo ambayo ilianza Januari 31 mwaka huu, iliandaa uzinduzi wake rasmi ambapo mgeni wa heshima alikuwa ni Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Mwanaidi Maajar na pia ilihusisha "maonesho" na maelezo ya bidhaa toka kwa wadau wahusikao na jamii ya Watanzania hapa nchini (kama Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika), mwanamitindo maarufu nchini Tanzania mama Asia Idarous na wajasiriamali wengi sana waTanzania wafanyao shughuli zao hapa nchini.

Mara baada ya kuwasili ukumbini, Balozi Maajar alipata nafasi ya kutembelea meza zote za maonesho na maelezo na kuchukua mawasiliano ya wajasiriamali hao, huku akisisitiza kuwaunganisha katika mtandao mmoja kupitia ubalozi katika kufanikisha lengo lao.

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©