Wiki
kadhaa zilizopita tuliwataarifu kuhusu
chombo tulichokitengeneza, TZelect —
Chombo cha Ushahidi, ambacho kitatumiwa
kukusanya na kujadili taarifa na ripoti
wakati wa Uchaguzi Mkuu.
Siku
chache zilizopita tulipata ujumbe kutoka
kwa vikundi kadhaa ambavyo vimeamua
kutengeneza chombo kingine (kinachofanana
na TZelect),
Uchaguzi Tanzania, ambacho
kitawezesha watu kuripoti kwa njia ya
kutuma ujumbe mfupi (SMS).
Vyombo
vyote viwili, TZelect na Uchaguzi
Tanzania, vinalenga Uchaguzi Mkuu wa
Tanzania utakaofanyika tarehe 31 Oktoba
mwaka huu, na pia kufuatilia
watakaochaguliwa katika kipindi
kinachofuata hapo baadae.
Malengo
haswa ya chombo cha Uchaguzi Tanzania ni
kutoa haraka taarifa zilizoripotiwa na
wananchi Tanzania. Na kwa upande
mwingine, TZelect itakuwa inakusanya
taarifa, maoni na mawazo; ni matarajio
yetu kuwa chombo hiki kitawapa jukwaa
watu — hasa vijana — kuanzisha mijadala
na kueneza ujuzi wa mchakato wa uchaguzi
na matukio mbalimbali.
Tunapenda
kuwakumbusha jinsi ya kuripoti; kwa njia
yoyote ile utakayotaka:
Jinsi ya kuripoti — TZelect
-
Kwa kutuma barua pepe (email):
tzelect
(at) gmail (dot) com
-
Kwa kutumia twitter na hashtags
zifuatazo:
#TZelect or
#uchaguzitz
-
Kwa
kujaza fomu kwenye tovuti
Jinsi ya kuripoti — Uchaguzi Tanzania
-
Kwa
kutuma ujumbe mfupi (SMS): 15540
-
Kwa kutuma barua pepe (email):
elections.tz (at) gmail (dot)
com
-
Kwa kutumia twitter na hashtags
zifuatazo:
#uchaguzi or
#humanrightstz
-
Kwa
kujaza fomu kwenye tovuti
Kama
unahusika au unajua miradi ambayo
inatumia teknolojia kama hizi kukusanya
taarifa na maoni kutoka kwa umma wakati
wa uchaguzi,
usisite kuwasiliana nasi ili
kuangalia kama kuna uwezekano wa
kushirikiana.